Wednesday, 18 December 2013

WANACHAMA SIMBA WATWANGANA JANA

Dar es Salaam. Pepo mbaya amezidi kuiandama Simba baada ya wanachama wanaodhaniwa kuwa wa klabu hiyo wanaotoka katika Matawi ya Mpira Pesa na Mpira Maendeleo kutwangana ngumi hadharani.
Tukio hilo lilitokea jana asubuhi mtaa wa Msimbazi yalipo makao makuu ya Klabu ya Simba ambapo uchunguzi wa Mwananchi ulibaini chanzo ni tofauti za kimsimamo baina ya wanachama wa matawi hayo mawili.
Mwananchi baada ya kufuatilia kwa kina lilibaini kuwa wanachama wa Tawi la Mpira Pesa wanataka Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Rage ajiuzulu kwanza wakati Mpira Maendeleo wanataka Kamati ya Utendaji nzima ya iondoke madarakani.
Hata hivyo, purukushani hizo zilikoma baada ya polisi kufika eneo hilo na kuingilia kati kuyatawanya makundi hayo.
Kumekuwapo kwa mijadala miongoni mwa wanachama na mashabiki wa Simba tangu mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo, Emmanuel Okwi aliposaini mkataba wa miaka miwili na nusu kujiunga na Yanga akitokea SC Villa ya Uganda ambayo alikuwa anaichezea kwa mkataba maalumu wa miezi sita.
Wanachama na mashabiki wa Simba wamekuwa wakihoji kulikoni Okwi asajiliwe na Yanga wakati klabu yao bado inaidai klabu ya Etole Du Saleh Dola 300,000 za mauzo ya mchezaji huyo ambazo bado hawajalipwa

No comments:

Post a Comment