Thursday, 12 December 2013

TWITE: KASEJA KAIMARISHA ULINZI

Juma Kaseja 

KIRAKA wa Yanga, Mnyarwanda Mbuyu Twite amesema yupo vizuri kimazoezi tayari kwa lolote huku akitamba kuwa kikosi chao kimeongezewa nguvu na kipa Juma Kaseja.
Mbuyu, ambaye kikosini hapo anachezeshwa kama beki wa kulia, ingawa mara nyingine anacheza nafasi ya beki wa kati, kushoto na kiungo hakuitwa kwenye kikosi cha Rwanda ‘Amavubi’ badala yake alibaki Dar es Salaam kwa mapumziko.
Aliliambia Mwanaspoti kuwa: “Kama unavyoona tunafanya mazoezi, ndiyo tunajiandaa taratibu, binafsi najiona niko fiti kwa sababu najua wajibu wangu, nimejiandaa na niko tayari kwa kazi.”
Akimzungumzia, Kaseja kuwepo kikosini mwao, Mbuyu alisema: “Kaseja ni kipa mzuri na hata kwenye mazoezi unaona, uwepo wake utaisaidia timu nzima na hasa safu yetu ya ulinzi kuhakikisha haturuhusu bao.

No comments:

Post a Comment