
Kocha wa zamani wa Yanga, Kosta Papic
KOCHA wa zamani wa Yanga, Kosta Papic amemponda Juma Kaseja kwa kujiunga na klabu hiyo ya Jangwani na kumuita kigeugeu.
Papic, ambaye sasa ni Kocha Mkuu wa Black Leopards
ya Afrika Kusini inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, alisema
alichokifanya Kaseja ni kukosa msimamo.
Kocha huyo wa Serbia alifafanua kuwa Kaseja
aliwahi kusajiliwa Yanga na kudumu nayo msimu mmoja wa 2008/09 kabla ya
kuondoka baada ya pande zote mbili kutoridhika.
“Alipokuwa Yanga aliondoka baada ya msimu mmoja na
alisema kuwa hakufurahia maisha ya Jangwani, sasa ni lini ameona maisha
ya huko yamekuwa mazuri, binafsi nadhani amekosea, hakustahili kwenda
sehemu ambayo amewahi kusema hana furaha,” alisema Papic, ambaye
alijiunga Yanga wakati Kaseja akiwa amerejea Simba.
Huku akimponda Kaseja kwa kujiunga na Yanga, Papic amemsifu Yaw Berko kwa kujiunga na Simba na kusema atawasaidia sana.
“Huyo Berko nakubaliana naye kwa sababu Yanga
walimuacha na kumuona hafai, lakini naye kama angekuwa amewahi kuchezea
Simba nisingekubaliana naye, ila kwa sababu anajiunga nayo kwa mara ya
kwanza nasema atawasaidia sana Simba,” alisema Papic alipozungumza na
Mwanaspoti kutoka Polokwane, Afrika Kusini.
Papic ndiye aliyesamsajili Berko msimu wa 2009/10
baada ya kumtoa katika klabu ya Liberty Professionals ya Ghana ambako
yeye alikuwa kocha wa Hearts of Oak ya mjini Accra.
Papic amewahi kufundisha Kaizer Chiefs, Maritzburg
United, Orlando Pirates za Afrika Kusini ; Lobi Stars, Enyimba, Enugu
Rangers na Kwara United za Nigeria.
Desemba 2008 alikwenda Ghana ambako alijiunga na
Heart of Oak mpaka Julai 2009 alipoondoka na kujiunga na Yanga ya Dar es
Salaam kwa vipindi viwili tofauti.
No comments:
Post a Comment