Tuesday, 17 December 2013

SIMBA KULIPELEKA SAKATA LA OKWI FIFA
















Dar es Salaam. Siku moja baada ya Yanga kutangaza  kumsajili mshambuliaji Emmanuel Okwi, uongozi wa Simba umesema hauna ugomvi na mchezaji  huyo licha ya kudai kufuatilia suala hilo Shirikisho la Soka Duniani (Fifa).
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ alisema wanachojua suala lao lipo Fifa na kama Yanga wamemsajili hiyo ni shauri yao kwani uamuzi ya Fifa kuhusu malalamiko yao bado haujatolewa.
“Etoel walimshtaki Okwi kwa Fifa, Okwi akawaeleza wazi yeye hajalipwa mshahara wake miezi mitatu, pia miezi mitatu hajacheza mechi hata moja ndiyo maana akaamua kuondoka, hivyo Fifa walimruhusu kucheza Villa.
“Hatuna kesi na Okwi tuna kesi na Etoil du Sahel watulipe fedha zetu, katibu (Evodius Mtawala) anafuatilia kuhakikisha tunapata majibu ya uhakika leo hii (jana) ili tujue moja na tutawajulisha kinachoendelea.” alisema Itang’are.
Jana Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema Okwi wamemsajili kwa muda wa miaka miwili na nusu na kuonyesha ITC ya mchezaji huyo iliyotolewa na Shirikisho la Soka la Uganda (FUFA) baada ya kupata baraka za SC Villa.

No comments:

Post a Comment