TIMU yake ya Manchester United inagaragara kwenye nafasi ya tisa katika msimamo wa Ligi Kuu England, lakini straika Wayne Rooney anashika namba moja kwa wanasoka raia wa Uingereza wanaotesa kwa utajiri katika ligi hiyo.
Kwenye orodha ya wanasoka 10 matajiri, mastaa Rio
Ferdinand, Frank Lampard, John Terry na Steven Gerrard wameingia ndani
ya tano bora, huku jina la staa wa West Ham United, Joe Cole
likiwaduwaza wengi kutokana na kuwamo kwenye orodha hiyo.
Wazawa wengine wenye pesa za nguvu kwenye Ligi Kuu
England ni Ashley Cole, Michael Carrick na Ashley Young, huku James
Milner akiwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi mwenye pesa kwa kuwa na
umri wa miaka 27.
Rooney anavyofunika
Akiwa na umri wa miaka 28, supastaa huyo wa
England soka lake limemfanya kuingiza pesa za nguvu na kuwaacha kwa
mbali Waingereza wenzake kwenye orodha hiyo.
Akiaminika kuwa na kipato kinachofikia Pauni 45
milioni, Rooney anapokea mshahara unaokadiriwa Pauni 250,000 kwa wiki na
kumiliki mikataba minono ya kibiashara ukiwamo wa kampuni ya Nike.
Kitokana na kipato chake, Rooney anamzidi mtu
anayeshika nafasi ya pili, Rio Ferdinand kwa tofauti ya Pauni 8 milioni
kutokana na beki huyo wa kati wa Manchester United kumiliki Pauni 37
milioni.
Rio anavuna pesa kupitia mgahawa
Kwa wanasoka Waingereza wenye pesa na wanaoendelea
kung’ara kwenye soka, Ferdinand anatajwa kuwa na kipato cha
kinachofikia Pauni 37 milioni, ambazo amekipata kupitia mshahara wake
anaolipwa Manchester United na biashara yake ya mgahawa pamoja na
jarida.
Staa huyo anamiliki mgahawa wake unaoitwa Rosso
uliopo jijini Manchester unamfanya apige pesa nyingi zaidi ukiweka kando
kipato kingine anachokiingiza kutokana na jarida lake la #5.
Kuwekeza kwenye miradi ya biashara ni kitu
kinachomfanya Rio kupiga pesa za maana licha ya sasa soka lake kuelekea
ukingoni kutokana na kuwa na umri wa miaka 35.
No comments:
Post a Comment