Wednesday, 18 December 2013

Luis Suarez: TUKIENDELEA HIVI UBINGWA WETU


Liverpool, England. Mshambuliaji Uruguay, Luis Suarez amekiri kuwa sasa amefanikiwa kuzikonga nyoyo za mashabiki wa Liverpool baada ya kupitia katika kipindi kigumu mwaka huu.
Jumatatu, Suarez ameshinda  tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2013 ya William Hill Football Supporters’ inayotolewa na Shirikisho la Mashabiki wa soka England.
Akipokea tuzo hiyo Suarez alisema “Liverpool najua kwamba hadi Januari tutakuwa tukiwania kuendelea kubaki katika nne bora, pamoja na kusaka ubingwa.”
Suarez alizikosa mechi sita za mwanzo wa msimu huu kutokana na kufungiwa April kwa kitendo chake cha kumng’ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic.
Tangu amerejea uwanjani tayari ameshafunga mabao 17, pamoja na kuiongoza Liverpool kuisambaratisha Tottenham kwa mabao 5-0 Jumapili.
Kikosi cha Brendan Rodgers sasa kitaivaa Cardiff, Manchester City na Chelsea kabla ya kumaliza mwaka huu na Suarez amekiri kuwa mechi hizo ndizo zitakazoamua hatima ya Liverpool katika kusaka ubingwa.
“Nafikiri ni rahisi sana kusema,” alisema nyota huyo mwenye miaka 26, wakati alipoulizwa kuhusu nafasi ya Liverpool katika Ligi Kuu.
“Kama tutaendelea kucheza kwa kiwango hiki katika wiki mbili au tatu zijazo hakuna shaka kwamba tunaweza kutwaa ubingwa wa ligi au kumaliza katika nne bora.
“Jambo la muhimu ni sisi kuendelea kuweka mawazo yetu katika mchezo unaokuja.
“Tunajua baada ya mechi ya Cardiff, tunamechi mbili ngumu zaidi.
Suarez pia aliwashukuru mashabiki wa Liverpool kwa kuonyesha imani kwake baada ya kufungiwa, amekiri kuwa asingeweza kuendelea kuwepo klabu hapo kama si wao kumuunga mkono.
Alisema: “Kurudi kucheza tena Anfield baada ya kupita katika kipindi kigumu hiyo yote inatokana na mashabiki kuwa nyuma yangu, ni kitu ambacho nilikuwa sikitegemei kabisa wakati niliporudi uwanjani.

No comments:

Post a Comment